AKUTWA AMEFARIKI KATIKATI YA BARABARA ENEO LA LITETA - MINGOYO, LINDI

akutwa amefariki barabarani
Kijana mmoja ambaye hakuweza kujulikana mara moja jina wala wapi anapoishi amekutwa amefariki katika Kata ya Mingoyo Manispaa ya Lindi katika eneo la Liteta.
akutwa amefariki barabarani
Kijana huyo aliweza kuokotwa alfajri ya leo katikati mwa barabara kuu na baada ya kumchunguza ilibainika ameshafariki na Mwili wake ukiwa unamajeraha hasa Sehemu ya Kichwani na kuonesha kuwa Kijana huyo aligongwa na Gari Majira ya Alfajiri.
akutwa amefariki barabarani
Kamanda wa Polisi wa Kituo cha polisi cha Mingoyo Juma Solomon ameweza kuthibitisha tukio hilo na kusema hadi sasa halijajulikana ni gari gani lililoMgonga mtu huyo. Hivyo uchunguzi Bado unaendelea.
akutwa amefariki barabarani
Naye Mtendaji wa Kata hiyo ya Mingoyo Bi. Maimuna H. Kawimba aliweza Kutoa taarifa kwa wakazi wa Kata hiyo kupitia kwa watendaji wa Vijiji waweze kuwataarifu wananchi/wakazi wa Kata hiyo Kuja kuutambua Mwili wa marehemu Kabla ya Kupelekwa Hospitali ya Mkoa Sokoine Baada ya Kukosa Ndugu aliyeweza kumtambua.
akutwa amefariki barabarani

akutwa amefariki barabarani

akutwa amefariki barabarani
Hadi sasa Mwili wa Marehemu huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa ya Lindi ya Sokoine hadi hapo ndugu watakapojitokeza kuutambua mwili wa marehemu.
akutwa amefariki barabarani

1 Comments

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post