Unknown Unknown Author
Title: WANAHABARI MKOA WA LINDI WAADHIMISHA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI KWA KUTOA MSAADA KWA JAMII
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa Habari Lindi akipimwa afya yake na daktari wa NHIF Timoth Mwasajone katika kuadhimisha siku ya Uhuru...
Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa Habari Lindi akipimwa afya yake na daktari wa NHIF Timoth Mwasajone katika kuadhimisha siku ya Uhuru wa Habari.
PICHA Ya Pamoja kati ya waandishi wa habari na wafanyakazi wa Mfuko wa NHIF Mara baada ya mfuko huo kujitolea kupima Afya za waandishi wa Lindi
Mwandishi wa Tbc Lindi Martina Ngulumbi akimpokea mtoto mama alietoka kujifungua siku ya uhuru wa habari
Mwenyekiti wa LPC ,Abdulaziz Ahmeid akikabidhi msaada Kwa Muuguzi wa zamu Bi Habiba Chitanda msaada uliotolewa na Wanahabari wa Lindi
Mwenyekiti akisalimia baadhi ya watoto wanaogua katika wodi ya watoto Sokoine Hosp mara baada ya kukabidhi vifaa mbalimbali katika kusaidia jamii siku ya uhuru wa habari

WANAHABARI  mkoa  wa  Wa Lindi wakiongozwa na Mwenyekiti wao wameadhimisha  siku ya uhuru wa  vyombo  vya habari duniani kwa kutoa msaada kwa jamiii baada ya kutoa msaada wa Vifaa mbalimbali katika wodi za wazazi na watoto katika Hospital ya Rufaa ya Sokoine Mkoani Lindi

Sambamba na  wanahabari  hao  kushiriki katika kutoa msaada huo pia wanahabari hao waliwezeshwa kupimwa Afya zao na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani humo ili kila mmoja afanye kazi zake huku akijua Afya yake

Akiongea baada ya hafla hizo,Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani Humo,Abdulaziz Ahmeid alieleza kuwa katika maadhimisho hayo ambayo kitaifa yamefanyika mkoani Arusha ambayo yana kauli mbiu ya Uhuru wa Habari kwa maendeleo na  utawala  bora Ambapo wanahabari wameamua kurudi kwa jamiii kwa kuona umuhimu wa kusaidia wagonjwa,Wazee na Walemavu

Ni Vyema waandishi tukajenga Utayari wa kusaidia Jamii na ndizo zenye Uhitaji wa misaada muhimu na hata kihabari kuliko kujikita na wanasiasa kwa maslahi yao na wakati wao tu Muhimu Tujitambue tutetee haki zetu ikiwemo Kuajiriwa na kufungwa kwa mikataba kuliko ilivyo sasa zaidi ya asilimia 90 HATUJIELEWI
Sambamba na hilo Tujikite katika kuandika habari za Uchunguzi na fursa zipo kupitia TMF..Alimalizia Abdulaziz


Nae Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Lindi Bi Fortunata Kullaya ambae alikuwa Mgeni Rasmi katika sherehe hizo zilizokutanisha waandishi toka wilaya zote za mkoa wa Lindi aliwataka
Waandishi kuandika habari kwa kufuata maadili ili wasijiingize katika matatizo hasa katika kipindi hiki cha mchakato wa katiba na kuelekea katika uchaguzi mkuu hapo mwakani kwa  kuwa wanahabari ni watu muhimu katika jamii  pia aliwataka kufika vijijini kubaini baadhi ya changamoto ambapo pia aliwahakikishia kuwa Mfuko wa Afya ya Jamii CHF sasa ndio mkombozi wa huduma za afya hivyo pelekeni Ujumbe Jamii
Ijiunge na ipate Tiba kwa Unafuu zaidi.


"Nyie ni wadau wakubwa wa NHIF, hivyo mbaini kuwa kalamu zenu zinaweza kujenga au kubomoa hivyo bima ya afya Tawi  Lindi  Tumeona ni siku muhimu sana kujumuika pamoja kwa kuwapima afya zenu ili mfanye kazi mkijijua".


Aidha katika maadhimisho hayo pamoja na kutoa msaada kwa Wagonjwa wa hospital ya Rufaa ya Sokoine na kupimwa kwa Afya za Waandishi kulifuatiwa na Tafrija Fupi ya Kutakiana heri iliyojumuisha waandishi na
wenza wao pamoja na wadau wengine wa habari iliyofanyika katika Fukwe za Santorin Beach Manispaa ya Lindi.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top