WAYNE ROONEY AWA NA HOFU TENA, NI UJIO WA KOCHA LOUIS VAN GAAL OLDTRAFOD

Na. Paul Manjale
Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Wayne Rooney ameigia hofu baada ya klabu hiyo kuwa na mpango wa kumuajiri muholanzi Louis Van Gaal kama kocha wake mpya baada ya Timu hiyo kumtimua David Moyes.

Hofu hiyo ya Rooney inatokana na uhusiano mzuri uliopo kati ya kocha huyo na mshambuliaji muholanzi aliyepo klabuni hapo Robin Van Persie.

Rooney anahisi uwepo wa kocha huyo Manchester United utamrudisha katika kumbukumbu za msimu wa mwisho wa kocha Alex Ferguson.

Ambapo alishuhudia Robin Van Persie akiwa ndiye mshambuliaji chaguo la kwanza huku yeye (Rooney) akiwa chaguo la pili na nyakati flani flani akianzia benchi.

Tusubiri tuone kama mambo yatakuwa yaleyale ama tofauti itakuwepo..

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post