NISHER ATAJWA KUWA MUIGIZAJI WA KIKE KINARA KULIKO WOTE BONGO MOVIE'S

clip_image001'Nisha Bebee'

HIVI karibuni kumekuwa na ubishani kwa mashabiki wa waigizaji wa kike Bongo Movie's,
Hatimaye kura nyingi kumdondokea dada huyu anaebadilika badilika katika husika za uchezaji wa filamu hadi kujikuta akihimili vishindo vya uchekeshaji wakati hicho ni kitu kigumu kwa wadada warembo kujitoa kufanya Comedy.

Tathmini iligundulika kwamba kwa sasa kinara ni Nisha Bebee baada ya kazi alizofanya kufanya vizuri katika soko la Filamu hapa nchini na Africa mashariki kwa ujumla.

Wengi walisema kuwa huwenda kile kimsemo cha dadididadiiiiiii.! alichokisema kwenye Filamu yake iitwayo TIKISA aliyomshikisha gwiji wa Vichekesho hapa nchini Amri Athumani King Majuto ndicho kilichomuongezea point.

Ama kweli kipaji acheni kiitwe kipaji.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post