KONGAMANO LA VIONGOZI WA DINI MKOA WA LINDI NA MTWARA LAANZA HII LEO

GESI 2Katibu mkuu wa wizara ya Nishati na Madini,Eliakim Maswi akiongozana na Viongozi wa Dini walipokuwa wakikagua mradi wa Gesi katika eneo la Msimbati.GESI 3Baadhi ya wanahabari wakiteta na Katibu mkuu wa nishati na madini mara baada ya kuwasili katika eneo la Madimba kukagua ujenzi wa sehemu ya kuchakata gesi na majumba ya wafanya kaziGESI 8Viongozi wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Lindi na Mtwara wakibadilishana mawazo na katibu mkuu wa nishati na madini.GESI 7Waandishi wa habari wakiwa katika basi kuelekea eneo la msimbati na Madimba kwa ajili ya kujionea mitambo ya gesi na ujenzi
unaoendelea katika vijiji vya msimbati na Madimba

Na Abdulaziz Video,Mtwara
Kongamano kubwa la Viongozi wa Dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara lililoandaliwa na Wizara ya Nishati na Madini limeanza leo katika manispaa ya Mtwara/mikindani kwa Viongozi hao pamoja na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kwa kutembelea eneo la Mnazibay/Msimbati sehemu ambayo imegundulika gesi asilia pamoja kukagua ujenzi wa eneo la uchakataji wa Gesi hiyo.GESI 4
Katika ukaguzi huo Viongozi hao wakiongozwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Bw Eliakim Maswi baada ya kuzungukia miradi mbalimbali ya Gesi na Mafuta kesho kutafanyika kongamano litakaloshirikisha Viongozi hao wa Dini na Viongozi wa serikali akiwemo mkuu wa mkoa wa Lindi na Mtwara.

Kauli mbiu ya kongamano hilo ni RASILIMALI ZETU ZA GESI ASILIA, MAFUTA NA MADINI KWA AMANI NA MAENDELEO YA TAIFAGESI 5Kongamano hilo linashirikisha zaidi ya wadau 200 kutoka mikoa hiyo ya Lindi na Mtwara wakiwemo maofisa wa wizara na serikali za mikoa hiyo pamoja na wanahabari

Habari zaidi na picha za kongamano litakaloendelea tutawajuza kupitia
Hapa Hapa hivyo usisite kutembelea globu yenu ya Jamii.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post