SHULE YA SEKONDARI YA ILULU YAPATA MSAADA WA VITABU KUTOKA AIRTEL VYENYE THAMANI YA TSH MILIONI 5

clip_image002[10]Meneja masoko wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kanda ya kusini na mkoa wa Morogoro Aminata Keita akikabidhi baadhi ya Vitabu vilivyotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa Salma Hamisi ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Ilulu iliyopo mkoani Lindi. Airtel ilitoa vitabu vyenye thamani ya shilingi Milioni tano kwa shule hiyo.

clip_image002[8]Meneja masoko wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kanda ya kusini na mkoa wa Morogoro Aminata Keita akimkabidhi Bernard Swai ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze. Airtel ilitoa vitabu vyenye thamani ya shilingi milioni tano kwa shule hiyo.

clip_image002[6]Meneja masoko wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kanda ya kusini na mkoa wa Morogoro Aminata Keita akimkabidhi Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule ya sekondari ya Chalinze iliyopo mkoani Pwani baadhi ya vitabu vilivyotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa shule ya sekondari Chalinze. Wanaoshuhudia katikati ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Emmanuel Kahabi pamoja na msimamizi wa bodi ya shule hiyo Bw. Mzee Madeni.

clip_image002Meneja masoko wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kanda ya kusini na mkoa wa Morogoro Aminata Keita akiwaelekeza jambo watoto wa shule ya sekondari Nanyamba iliyopo Mkoani Mtwara ikiwa ni muda mfupi baada ya kampuni ya mitandao ya simu za mkononi Airtel kukabidhi vitabu vyenye thamani ya shilingi milioni tano kwa shule hiyo ya sekondari.

SOURCE: MICHUZIJR BLOG

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post