JESHI Polisi Mkoani Mtwara limefanikiwa kukamata gari lenye namba za usajili T867 aina ya Toyota Carina Saloon likiwa limebeba shehena ya mifuko yenye meno ya Tembo tisini (90) yenye uzito wa kilogramu 222.1 ya thamani zaidi ya shilingi bilioni moja (1,082, 025,000/=)
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Zelothe Steven alisema kuwa gari hilo lilikamatwa kata ya Maendeleo, wilaya ya Masasi katika barabara kuu ya Tunduru kuelekea Masasi.
Zelothe alisema kuwa askari wa doria walilitilia shaka gari hilo na kumuamuru dereva kusimama kuonyesha leseni ya udereva ambapo dereva wa gari hilo hakuwa nayo, ndipo askari alichukua hatua ya kufanya ukaguzi ambapo alikuta gari hilo limejaza shehena ya mifuko inayosadikiwa kuwa ni meno ya Tembo.
“Askari waliamua kulifikisha gari hilo kwenye kituo kikuu cha Polisi wilaya ya Masasi umbali wa kilometa moja kutoka sehemu lilipokamatwa gari hilo, wakati wakiwa njiani kuelekea kituoni dereva na mwenzake walikuwa wakimshawishi askari huyo waelewane ili wampatie shilingi milioni tatu aweze kuwaachia lakini askari huyo alikataa na kufanikiwa kulifikisha gari hiyo kituoni” Alisema Zelothe.
Alisema kuwa kabla gari hilo halijasimama vizuri dereva na mwenzake waliruka na kutokomea vichochoroni, juhudi za kuwasaka bado zinaendelea ili waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani.
Miongoni mwa vitu vilivyokutwa ndani ya gari hilo wakati wa upekuzi ni pamoja na simu moja ya kiganjani aina ya Techno, mizani aina ya tonash, fomu za “notification” pamoja na Bank slip.
Swali langu ...Watuhumiwa wameruka au Mshiko umefanya kazi kwa Polisi? Nina mashaka…..