SUAREZ AKANA KUSEMA ANATAKA KUBAKI LIVERPOOL

clip_image001Suarez alikuwepo kwenye kikosi cha Uruguay leo kilichoifunga Japan 4-2

MSHAMBULIAJI aliye katika wakati mgumu, Luis Suarez amekanusha taarirfa kwamba leo alisema yuko tayari kurudi kazini na kubaki Liverpool.

Mchezaji huyo anayetakiwa na Arsenal amenukuliwa katika mahojiano kutoka nchini Japan na gazeti la Uruguay, El Observador akisema angebaki Anfield kwa sababu ya jinsi aanvyoungwa mkono na mashabiki wa Liverpool.

Lakini akizungumza baada ya kuiwezesha Uruguay kuifunga Japan 4-2 katika mchezo wa kirafiki, Suarez alikanusha na kusema hajabadilisha moyo wake.

"Sikusema hivyo, labda mtu mwingine alifanya hivyo na kitu cha msingi ni kwamba, nipo hapa kwa sasa na timu ya taifa," Shirika la Habari la Japan, Kyodo limenukuu akisema.

clip_image001[6]Suarez (kushoto) akishangilia na mshambuliaji pacha wake, Diego Forlan baada ya kuifungia bao la tatu Uruguayclip_image001[8]Katika mpambano kamili: Suarez alidaiwa kusema upendo wa mashabiki unamfanya abaki, kabla ya kukanusha taarifa hizo

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post