SIMULIZI: “USILIE NADIA” SEHEMU YA KUMI NA NANE

clip_image003SIMULIZI YA MAISHA: USILIE NADIA
MTUNZI: George Iron Mosenya
SMS: 0655 727325
SEHEMU YA KUMI NA NANE
Wanasema kuwa baada ya dhiki ni faraja lakini kwa Nadia mimi kila baada ya dhiki ilikuwa inakuja dhiki nyingine inayofanana na faraja kisha inanisulubu. Hata hapa nilipokuwa sikutaka kujidanganya kuwa nimefika katika kikomo cha mateso!! Lakini walau nilikuwa katika mikono ya Jesca, na hapo niliweza tena ku….” Nadia akanitazama kisha akatabasamu!! Nikaelewa alikuwa anamaanisha nini kuikatisha ile kauli.
“Hee!! Yaani kumbe unanisikiliza tu hata kusema Nadia twende kula muda umefika aa mwanaume mbaya wewe dah!! Mwone!! Mi nina njaa mwenzako sio siri, ile kapuchino yote imamemalizika tumboni…”
“Niwapigie simu walete huku ama..”
“Hamna hawa wakileta huku huwa wanapunja sana. Twende hukohuko yaani wakinipunja tu naenda jikoni mwenyewe kujipakulia.” Alitania Nadia, tukajikuta tunacheka wote.
“Haya basi nipishe nibadili nguo mwenzako.’ Aliniomba, nami nikatoka nje ya chumba chake na kwenda katika chumba changu.
Huko chumbani wakati na mimi nabadili nguo nilikuwa nahangaika na utata wa simulizi hiyo yenye maswali mengi!!
Sasa Jesa na Nadia wamekutana Dar!! Hivi huu ndo mwisho wa simulizi ama? Lakini haiwezi kuisha maana hali niliyomkuta nayo Nadia Musoma haikuwa ya kawaida hata kidogo sasa alirudi lini Musoma na ni kwanini nilimkuta katika hali ile??
**HAYA KESHO ataendelea kusimulia bila shaka tukimaliza kula ataendelea!!!!
TOA MAONI YAKO!!! BOFYA LIKE kama tupo sambamba
Baada ya dakika zipatazo kumi mlango wangu uligongwa nami wakati huo nilikuwa namalizia kufunga kishikizo katika shati langu.
Nikauendea mlango huku nikijua kuwa lazima atakuwa Nadia, na sikuwa nimekosea alikuwa ni yeye.
Nikaufunga mlango kisha kwa mara nyingine tukaenda chini kupata chakula.
Nadia akaagiza nami nikaagiza, baada ya muhudumu kuondoka nikamtazama Nadia na hapo nikapata cha kuanzia maongezi maana tulikuwa kimya sana.
“Yaani macho yako dah! Yamekuwa mekundu, ukiongezea huo weupe na kilio ndo umetisha kabisa.”
“Duh nimejaribu kunawa, bado yanaonekana mekundu?” akanijibu. Nikamweleza kuwa si tu mekundu bali yamevimba pia. Kisha nikaongezea neno ambalo lilizua simulizi nyingine kutoka kwa Nadia.
“Aisee kama yangekuwepo mashindano ya kulia duniani ungejitwalia tunzo.” Nadia akanitazama kwa makini kama vile hakusikia vyema nilichomweleza.
“Katika hayo mashindano labda kama Jesca asingeshiriki. Lakini kama angeshiriki basi tena kila mashindano yanapofika angeshinda yeye, aisee kuna watu wanajua kulia duniani, sema heri yake yeye ni mweusi hata hawi mwekundu, tatizo moja tu akilia mwache hadi anyamaze hataki kubembelezwa na mbaya zaidi anaweza hata kukutusi ukijifanya kumbembeleza, dah Jesca!! Lakini alikuwa na sababu ya kulia, na ni Jesca anayenifanya nizidi kuamini wanaume wote ni sawa tu hakuna cha wewe mwandishi wala raisi wa nchi wote hamna maana kabisa, yaani ujue siku ya kwanza namwona Bryan nilimwona tu kama vile kuna jambo analificha, niliona kabisa tabasamu la kinafiki kutoka katika uso wake, nami nikampa tabasamu la kinafiki maisha yakaendelea. Wakanifiokisha hadi mahali walipokuwa wanaishi, aisee nitakuwa mnafiki nikisema Bryan nalikuwa hajajipanga, kiukweli alikuwa amekamilisha kila kitu kinachofaa kuwa ndani ya nyumba, na Jesca alikuwa mama mwenye nyumba ile.
Nilipofika pale mida ya jioni nikatambua kuwa jumla ndani tulikuwa watu hai watano, Jesca na mchumba wake, msichana wa kazi na kitoto kidogo, na mimi. Jesca akanieleza kuwa alizaa kabla ya kuingia chuo. Sikutaka kumuhoji sana lakini ni kama alikuwa na simulizi nyingine nzito nyuma yake. Nikaandaliwa chakula nikala na hapo nikapata nguvu mwilini.
Siku iliyofuata nilibaki mimi na msichana wa kazi na mtoto, Jesca alienda chuo na mchumba wake alienda alipojua yeye. Hakika siku hiyo nilivuta hewa safi na kujisikia nipo nyumbani kabisa, siku ya pili na hatimaye majuma mawili nikiwa nakula milo mitatu kwa siku.
Ndipo ikafikia siku ya kupata majibu yangu!! Siku hii Jesca alichelewa sana kutoka chumbani mwake, na hata alipotoka alikuwa amevaa hijabu.
“Jesca wewe na hijabu wapi na wapi na tangu lini?” nikamuuliza. Badala ya kujibu akacheka tu!! Nikajua anapotezea kujibu swali langu, kiherehere kikanishika nikaendelea kuuliza.
“Mwenzangu, mara moja moja huwa navaa…” alinijibu kwa sauti ya chini na hapo hapo nikaona kitu cha kustua sana.
Damu!! Damu katika hijabu nyeupe ya Jesca.
“Jesca, na hiyo damu hapo!!”
“Wapi eeh!! Damu.” Akaweweseka nami nikamkazia macho. Sikumjibu weweseko lake nikamngoja aseme kitu.
Mara akaanza kulia!! Si nilikwambia kuna watu wanajua kulia mwandishi, alilia akakimbilia chumbani kwangu!! Nami nikamfuata.
Nikamkuta ameondoa hijabu na kichwa kimebaki wazi na alikuwa amejiinamia. Nikamtikisa, alikuwa analia tu!!
Mara akaunyanyua uso wake, mwandishi mimi najua nilishapigwa sana hata mara nya kwanza kuonana na wewe ulinikuta na majeraha lakini ni mara chache sana niliwahi kuona mtu amepigwa akapigika.
Jesca alikuwa hatamaniki kumtazama! Alikuwa na manundu usoni na katika paji la uso na alikuwa na michubuko kadhaa.
“Jesca ni nini ntena hiki?’ nilimuuliza lakini hakujibu bali alikuwa analia kama mtoto mdogo, alilia sana kila akijaribu kusema neno inashindikana anaambulia kutoa kamasi tu, kisha kilio upya, halafu analia kwa sauti ya juu sasa. Nikamwacha akalia kwa takribani nusu saa. Hapo sasa kidogo aliweza kusema neno la kwanza kuhusiana na uso wake.
“Bryan amenipiga Mariam, amenipiga sana jana usiku!!” sitaisahau sauti hii jinsi ilivyonichoma na kuniumiza moyo wangu. Chozi likanitoka nikawahi kulidaka kwa kutumia kitambaa cha mkononi, Jesca hakuona.
Jesca akanieleza juu ya maisha yake kwa miaka miwili nyuma. Akanieleza juu ya mjomba wake kushindwa kuendelea kumlipia ada kutokana na shinikizo la mkewe, kabla matokeo hayajatoka Jesca akazurura huku na kule na mwisho kukutana na Bryan, mwanaume ambaye alimpa sharti moja tu kuwa naye katika mapenzi kumzalia mtoto na kisha atamfanyia kila kitu.
Kwa sababu Jesca alipenda kusoma akakubaliana na hali, akabeba mimba akiwa nyumbani, baadaye Bryan akamtorosha kwenda Dar es salaam, ni huko ambapo alimzaa mtoto wake wa kwanza akiwa mwaka wa kwanza chuoni. Mapenzi yaliendelea vyema lakini unyanyasaji ukaanza taratibu kisha kukolea, Bryan akamfanya Jesca kama mtoto mdogo, hatakiwi kuulizia lolote ambalo atakuwa na mashaka nalo, hakuruhusiwa kujua Bryan anafanya kazi gani na wapi. Na baadaye vipigo pasipo na sababu vikaanza, Jesca akavumilia tu! Siku nyingine Bryan harudi siku tatu, akirudi siku ya nne asikute chakula mezani inakuwa tiketi ya kumpiga Jesca. Jesca hakuwa na la kufanya kwa sababu alikuwa mtumwa tu na alimtegemea Bryan kwa kila kitu, akipigwa anajikausha, akitukanwa hajibu kitu, nia yake ikiwa kumaliza masomo ya chuo kikuu na kutafuta kazi yake.
Kama hiyo haitoshi Bryan akaanza tabia mbaya kabisa, tabia ambayo baada ya kukataliwa nd’o ikanogesha kichapo kila siku. Yaani acha tu Mariam naishi kimateso sana hapa. Nd’o kama hivi akinipiga navaa hijabu naenda chuo, ipo siku nitatimiza ndoto zangu dada Mariam ipo siku na Mungu ninayemuamini ananisimamia”
“Jesca kuna jambo gani jingine la zaidi.” Nilimuuliza baada ya kuona maelezo yake yana walakini.
“Nikitoka chuo basi dadangu.” Akanijibu, akavaa hijabu nyingine, akaondoka!!
Mwandishi niliyapima yale maelezo ya Jesca lakini hayakuniingia akilini, niliamini kuwa lazima kuna jambo la ziada linasababisha haya, haiwezekani mwanaume akutoe kijijini huko akulete mjini akubali umzalie, akutafutie mfanyakazi akuweke katika nyumba kubwa mwisho aanze tu kukupiga, akili ikagoma.
Nikajiahidi kuwa akitoka chuo nitambana nijue alimkosea nini Bryan, nikahisi huenda hata aliwahi kumsaliti ama ana kimwanachuo kingine huko anarusha shutuma kwa Bryan!! Nikaingoja mida ifike.
Jioni ile akarejea akiongozana na mchumba wake!! Wakaenda chumabni moja kwa moja.
“Jesca mwambie Naomi asituwekee chakula tumekuja nacho sawa eeh!!” Bryan aliniambia kwa sauti tulivu, nikaitikia kwa kichwa.
Nikajua wapendanao wamepatana tayari!! Na nikaamini kuwa nimeikosa nafasi ya kujua nini kinamsibu Jesca.
Usilolijua mwandishi ni sawa na usiku wa giza……” akasita kidogo akatazama mahali nami nikatazama, muhudumu alikuwa analeta chakula.
“Vipi atupelekee chumbani ama vipi?” nilimuuliza Nadia.
“Yaani kama ulikuwa kichwani mwangu!!” alinijibu, nami nikachukua jukumu la kumweleza muhudumu nia yetu! Akatii.
Tukaenda chumbani!!
Tulikifunika kile chakula, Nadia akaendelea kuzungumza.
“Yaani sijui ni ule moyo wa Jadida bado ulikuwa ukikitawala kifua changu ama vipi, yaani sikuwa na amani hata kidogo, hadi majira ya saa tano usiku nilikuwa sijalala. Nilikuwa nikitafakari uhuni wa wanaume hawa. Nikajikuta nahisi nipo katika nyumba moja na Desmund!! Kwa aliyonisimulia Jesca nikamwona Bryan kama Desmund. Na hapo nikaanza kuwafananisha lakini nikashtushwa na kishindo kikubwa.
Ule ulikuwa usiku hivyo kishindo hata kama ni kidogo lazima ukisikia vyema, vipi kuhusu kishindo kikubwa.
Hapo nikavamiwa na akili ambayo naweza kuiita ya kitoto. Sikuwa nimebanwa mkojo lakini ile hali ya kujua kuwa njia ya kwenda chooni ni lazima upite mbele ya chumba cha Jesca na mchumba wake. Nikaamua kutoka kwenda chooni nikijisemea kuwa huenda ni Jesca amepigwa!!
He! Ujue ilikuwa kama masihara, napita mbele ya kile chumba nikawa nasikia mabishano, hakika yalikuwa mabishano makubwa!!
Jesca alisikika akilia, na Bryan alikuwa anakoroma akilazimisha jambo.
“Jessy nitakuua ujue, nitakuua nasema….si wewe huwa unakataa halafu nikienda kwa watu wengine unaleta kidomodomo. Si uwe unakaa kimya!! Sasa nasemaje leo ni utake usitake.” Kauli ikakatika kisha ikasikika kelele mithili ya mikanda, Jesca alikuwa anachapwa maana nilimsikia akilia sana na hapo akasema neno.
“Bryan we niue tu lakini mi sitaki hayo mambo sitaki Bryan mbona unakuwa huniheshimu?? Eeh!! Bryan mi sitakiiiiii…..” alilalamika . Hapo kiherehere changu kikanivuta kuchungulia kama inawezekana. Nikatazama kushoto na kulia, hakuna mtu!! Nikausogelea mlango, uzuri waliacha taa inawaka, kupitia kitasa nikakuta kitundu kidogo, nikajivika ujasiri na kuchungulia kidogo, kisha nikatoka kwa kunyata hadi chumba cha mfanyakazi nikamkuta anakoroma nikafunga kwa njue ili akibanwa mkojo na kutaka kutoka nje asiweze kunifumania, nikarudi tena kuchungulia.
Jesca alikuwa akilazimisha kuishika chupi yake, Bryan akawa anaivuta huku akimchapa kwa kutumia ule mkanda. Jesca alikuwa amechakaa vibaya kutokana na kipigo.
“Bryan mwanao anakuangalia ujue, kuwa na aibu Bryan unachotaka kufanya si Mungu wala mwanao anakipenda…acha Bryan acha!!” Jesca alizidi kusisitiza. Bryan akageuza jicho akatazama kitanda cha mtoto wao ambaye alikuwa amelala. Kisha akapuuza. Hapo sasa akatumia nguvu zaidi!!
Mimi nilikuwa sijapata jibu, Jesca ni kipi anachokataa.
Nikaendelea kuangalia filamu hiyo ya kutisha. Mara Bryan akafanikiwa kuitoa nguo pekee iliyobaki akatika mwili wa Jesca, mara akaitoa bukta yake!! Ningekuwa Nadia wa miaka ile ningeweza kustuka lakini Nadia huyu wa kuitwa Mariam hata sikutetemeka nikaendelea kuangalia. Na baada ya sekunde kadhaa nikapata jibu na hapo nikageuka Nadia mtata.
Maneno ya Jesca sitayasahau hata kidogo, ni haya yaliyonibadilisha ghafla usiku ule na kujikuta katika chuki isiyosemekana na kisha kunisukumia kufanya jambo ambalo lilinirudisha shimoni. Shimo la mateso.
“Bryan haujalewa na una akili zako timamu, sina nguvu za kukabiliana na wewe na unanifanyia haya mbele ya mtoto wako, kama nikidhurika Bryan mwanao pekee ndo shahidi kuwa si mimi niliyetaka bali umenilazimisha kuniingilia kinyume na maumbile!! Ni yeye atakayekuhukumu.” Jesca alimaliza kisha akamwacha Bryan afanye lolote lile ambalo alikuwa anataka kulifanya.
Ningekuwa mpumbavu kushuhudia haya!! Nilikuwa nimekula na nimeshiba, sikumwogopa tena Bryan. Na ili nimkabili vyema nikambatiza jina nikamuita Desmund!!
Bryan bila haya akachukua mafuta fulani mkononi na kumsogelea Jesca!!
Nikafanya jaribio!!
Jaribio lililofanikiwa, nikakishusha kitasa, mlango ukafunguka!!
Ana kwa na ana mtu na mpenzi wake wakiwa uchi wa mnyama!!
“We Mariam!!..we…” kigugumizi kikamshika Bryan.
“Endelea unachotaka kufanya Desmund!!” nikamwita kwa jina hilo ili nijitie hasira zaidi.
“We Mariam unaota ama nani Desmund hapa.” Jesca alijiongelesha kama vile hakuna ambalo lilitaka kutokea.
Bryan akajaribu kunisogelea na hapo ndipo nikatambua kuwa tabu nilizopitia zilinikomaza, nilimrukia Bryan nikambamiza kwa kutumia goti langu katika korodani zake. Nikaiona sura ya Desmund machoni pake!! Jesca akanisogelea nikamsukuma huko akaanguka, sasa nikaanza kumchapa na ule mkanda, akajaribu kusimama nikamkanyaga teke la tumboni. Akaanguka chini akatoa kilio nikasikia sauti kama ya Desmund!! Nikazidi kucharuka nikachukua chupa ya soda akataka kujitetea nikawa nimeirusha tayari ikambamiza kichwani, akarudi chini na kuiangukia sakafu kisha akatulia.
“Anataka kukudhalilisha na unataka kumtetea…unaijua thamani yako Jesca?? Unaijua??” nilimuhoji akawa anatetemeka badala ya kunijibu.
“Sasa unasimama muda huu na unaondoka hapa leo hii hii…”
“Lakini ni usiku …”
“Shhhh!! Nasema Jesca unaondoka hapa ama niondoke mimi na usije ukasema uliwahi kukutana na mimi katika maisha yako. Wewe ni mwanamke, unatakiwa kujitambua…unataka kuuchekea huu upuuzi!! Mwanao ataiiga nini kwako, unamuandaa kuwa shoga?” nilimuuliza kwa ghadhabu kuu….Jesca akawa mpole.
“Vipi sasa chuo?”
“Vyote vya shetani ni batili!! Bryan ni shetani mkubwa.” Nilimjibu!! Hapa sasa akanielewa.
“Si9 unazo pesa kidogo.”
“Zipo…”
“Tunaondoka hapa sasa hivi na mtoto. Aisga akiamka antakutana na mfanyakazi wake ama akifa jumla wazazi wake watakisia nini kilichomuua ama hao wanawake wake wajinga wajinga ambao huwa wanamtegemea mi*** yao watatoa taarifa kwa polisi.” Niliongea kwa ghadhabu sana na nilitukana, nadhani unanisamehe mwandishi maana nasema kilichotokea!!” Nadia aliniambia nikakubali kwa kichwa kisha akaendelea.
Ilikuwa saa sita usiku, nikambeba mtoto wa Jesca,tukatoka nje, jiji lilikuwa halijatulia bado. Tukapata taksi tukaondoka na kwenda kulala nyumba za kulala wageni huko Ubungo!!
Huu ukawa usiku wa namna yake mwandishi, usiku ambao niliamua kwa kauli moja tu, Mungu ananionyesha mabalaa haya, Mungu ananiepusha na kifo akiwa na maksudi nami, halafu ni kama nilikuwa nalaza damu.
Jesca alinieleza kuwa alikuwa na kiasi cha laki saba katika akaunti yake. Hii ilikuwa inatosha sana, ilikuwa ni wakati muafaka wa kumkabili Desmund ili nimpe salamu kutoka katika ile kuzimu ya baharini ambayo nilikuwa na kisha ikazushwa kuwa nimekufa.
Mzee Matata angeongoza mbio hizi za kunieleza ni nanji huyo alitaka kuniua kabla sijaonana na Desmund mume wangu, kila ambaye angenipa jibu hyakika angekuwa amenisaidia sana. Jesca na mwanaye walisinzia lakini mimi nilichelewa sana kulala.
Mwisho nikalala nikiwa na kauli mbiu, nipo hai ili Desmund akome!....mh!! we G wewe yaani ukinogewaga kusikiliza hata kula hunikumbushi au ndo unataka vidonda vya tumbo visimame hapa tuanze kukimbizana hospitali tena” alisema Nadia hapo nami nikakumbuka kuwa kulikuwa na chakula mbele yetu, nikakifunua.
Ewalaa!! Mapaja mawili ya kuku wa kienyeji, wali mweupe na vidikodiko vingine.
Nadia sahani yake na mimi yangu!!!
Kila mtu kwa mwendo wake akaanza kula!!
**NAAM!! NADIA amempigania Jesca asifanyiwe kitendo kile kiovu!! Sasa amemwamrisha na wameamua kuondoka…ndoto za Nadia kukabiliana na mheshimiwa diwani Desmund!! JE ATAFANIKIWA!!!!!!

***KESHO TENA MUNGU AKIPENDA***

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post