MADE IN TANZANIA, HATA SISI TUNAWEZA CHEKI GARI HILI

clip_image001Mwang'oka akiwa ndani ya gari lakeUmeuona mlango? Mwang'oka akishuka garini Akifunga mlangoAkionyesha siti ya abiria wakeJuu tumeweka kupitisha upepo

Umeona dashboard yake ilivyoMbunifu Kenneth Joseph Mwang'oka akiwa katika poziGari hilo linaloonekana kwa mbeleKishoka napiga hiviBomba la kutolea moshi ndilo hiliWatu wakilishangaa gaari hiloUmeona vitendea kazi vyakeUsukani wake ni mbao tu kweli msimu ni maliMuonekano wa gari hilo kwa nyumarivasi kama kawa TANZANIA imejaliwa watu wenye vipaji na ujuzi mkubwa katika nyanja ya Sayansi na Teknolojia ila kuna vitu vidogo vinavyowakwaza kusimama na kwenda sambamba na wataalam wa mataifa mengine ambao wapo mbali katika suala la vipaji na ubunifu.
Mifano michache ni watu wanaomudu kutengeneza magobole, mashine mbalimbali na vitu vingine na hata wabunifu wa mrusho wa matangazoi ya radio, ambao badala ya kuwezeshwa hupata vikwazo ikiwamo kunaswa na vyombo vya dola na kufunguliwa mashtaka ilihali wangeweza kutumika kuitangaza Tanzania.
Hapo juu ni mmoja wa wabunifu wa Kitanzania aliyeweza kutengeneza gari ambalo alitumia muda wa miezi sita kulikamilisha kwa kuokoteza vifaa na kulipambana kiasilia kwa kutumia malighafi ya misitu.
Majina yake kamili ni Kenneth Joseph Mwang'oka ambaye alikuwa moja ya vivutio katika Maonyesho ya Biashara ya Sabasaba kwa ubunifu wa gari hilo linalotumia injini ya Toyota na kuongeza ubunifu wao kiasi kwamba gari hilo lililomgharimu kiasi cha Sh Milioni 8.6 kutembea kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Mwenyeji huyo wa mkoa wa Mbeya, lakini ubunifu wake kaufanyia mjini Iringa anasema lengo lake ni kuhakikisha anakuja kuntengeneza vitu zaidi ya gari hilo la aina yake.


Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post