Baada ya kumpa shavu The Heavy Weight MC Profesa Jay kwenye joto hasira, Lady JayDee a.k.a Anaconda anaendeleza utamaduni wa kuwapa mashavu wasanii wakongwe na wakali..hivi karibuni alirekodi wimbo na Q chilah, and guess Who’s next, ni Juma Kassim Nature Kiroboto.
Kupitia akauunti yake ya twitter Anaconda amewapa fans wake good news kuhusu ujio wa ngoma yake na Juma Nature, huku akitaka kujua kama wako tayari kuipokea.
Jiwe jingine Jide na Sir Juma Nature. Mko tayareeee????
— Lady JayDee (@JideJaydee) July 19, 2013
fans wengi waliipokea habari hiyo kwa shangwe lakini Jide aliwaeleza kuwa sio kwamba kila wimbo anaorekodi sasa hivi atauachia sasa hivi.
“Tunarekodi tu nyimbo ili ziwepo ila haimaanishi zote zitatoka kwa wakati mmoja zitapeana muda. Wakati ukipata hisia lazma uingie Studio.” Alitweet Lady JayDee.
Kwa upande mwingine Mkali huyo aliweka wazi kile kinachomnyima amani katika maisha yake ‘kimuziki’ kuwa ni kiu ya kufanya wimbo na malkia wa mipasho Khadija Kopa.
Bado sijakamilisha ndoto nyingine ya kufanya wimbo na Khadija Kopa.. Roho yangu itasuuzika na nitaishi kwa amani baada ya hapo
— Lady JayDee (@JideJaydee) July 19, 2013
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.