JULIO APEWA MWAKA NDANI YA SIMBA

clip_image001Kocha mwenye maneno mengi nchini Jamhuri Kihwelo 'Julio' amepewa mkataba mpya na simba wa mwaka mmoja baada wa ule wa awali  wa miezi 6 kuhitimishwa hapo juzi.
Julio ataendelea kuwa msaidizi wa Abdalla Kibaden baada ya kupewa mkataba mpya na uongozi wa Simba SC utakao muweka katika benchi la ufundi la simba mpaka mwakani mwezi huu.
Akizungumza na moja ya redio hapa nchini hii leo Julio alisema kuwa anashangazwa na vyombo vya habari vilivyo ripoti kuwa hana chake ndani ya Simba SC, wakati mkataba wake wa awali ukikimbilia kuisha.
Julio alisema kuwa amesaini Simba mkataba wa mwaka mmoja na anamini atafanya kazi kubwa chini ya Abdallah King Kibaden Mputa katika kuliongoza benchi la ufundi la Simba SC.
Julio alisema kuwa wanataka kuwazodoa wale wanaosema makocha wazawa hawawezi fanya vizuri, na kuwataka mashabiki wangoje kuona kazi inayofanywa na Kibadeni na yeye ndani ya Simba SC.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post