David Moyes anataka kuimarisha safu yake ya kiungo kabla msimu mpya haujaanza Chaguo la kwanza: David Moyes anahitaji sana saini ya Cesc Fabregas at Barcelona wa Barcelona
Kama Manchester United watalipa zaidi ya pauni milioni 30, watakuwa wamevunja rekodi ya usajili wa klabu hiyo ambapo mpaka sasa usajili wa Dimitar Berbatov - wa pauni milioni 30.75 kutoka Fulham, mwezi septemba, 2008 unashikilia rekodi.
Moyes alipoulizwa kama ataangalia wachezaji wengi endapo atamkosa Fabregas, alikiri kuwa ndiyo, lakini kwa sasa hawezi kuongelea poiti hiyo kwani hajapanga bado.Muungano huo: Fabregas wanaweza kuungana tena na mchezaji mwenzake wa Arsenal, Robin van Persie (kulia)Wanaonekana poa sana: Shinji Kagawa (nyuma) akiwa na Danny Welbeck (kulia), David de Gea (katikati) na Patrice Evra wakati United walipotembelea duka la Paul Smith store mjini YokohamaInakufaa bwana mkubwa: De Gea akichagua nguo dukaniInauzwa! Wilfried Zaha akishika bagi wakiwa na muuzaji msaidiziBei gani? Rio Ferdinand akiangalia baadhi ya nguo dukani
Na Baraka Mpenja
Kocha wa Manchester United, David Moyes amethibitisha kuwa klabu yake imeshatuma ofa nyingine ya kutaka kumsajili kiungo mahiri wa Barcelona Cesc Fabregas na hayuko tayari kukata tamaa, bali ataendelea kuwashawishi wazee hao wa katalunya ili wamuachiea kifaa hicho.
Akiongea katika mkutano na waandishi wa habari dimba la Yokohama Nissan leo hii, Moyes amesema mkurugenzi mkuu wa United, Ed Woodward anaendelea kuzungumza na miamba hiyo ya Hispani kuhusu Fabregas baada ya kutuma ofa ya pili ya pauni milioni 30, lakini kwa sasa wataongeza mzigo mwingine na kuvunja rekodi ya klabu hiyo katika usajili.
Moyes Alisema: “Nafahamu Ed anawajibika kwa hilo na amekuwa akizungumza na Barcelona na kwa mara nyingine tumeandaa ofa ya pili. Lakini Ed ndio mhusika mkuu kuliko mimi binafsi”.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.