Basi la kampuni ya Hood lililokuwa likitoka Tunduma kernda Dar likijaribu kulipita lori katika kona kali za mlima KitongaHapa dereva wa basi hilo bila kujali usalama wa abiria wake akiendelea kutaka kupenya jambo ambalo ni hatari zaidiHapa akiwa katika harakati za kulipita Lori hilo Hapa basi hilo lenye namba T 751 AVL likinusurika kugongana uso kwa uso la basi la Sumry baada ya kulazimisha kulipita lori katika eneo la mlima Kitonga huku kukiwa na kona kali kiasi cha basi hilo kutaka kutumbukia katika korongo la mlima huo kama linavyoonekana kushoto, kazi ya usalama wa abiria na kudhibiti uzembe wa madereva kama hawa katika mlima Kitonga lipo mikononi mwa askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Iringa ambao mwaka jana waliagizwa na mkuu wa kikosi hicho Taifa Mohamed Mpinga kuweka askari eneo hilo ila wameonyesha kupuuzia.
PICHA KWA HISANI YA RICHARD-MWAIKENDA BLOG
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.