"Hii sasa ni zaidi ya hatari"....Be careful

Ilikuwa yapata mida ya saa kumi na mbili natoka ofisin nimebeba bag langu la laptop....ofsn kwetu ni karibu na chuo fulan cha uhasibu nikawa natembea miguu kwan sijabahatika kupata usafiri....
Wakati natafakari nikifika nipike nn kwan bado niko "bachelor", njian nikakutana na binti mrembo sana tena sana akawa anatembea anaelekea maeneo ya chuo...
    Bhana eeeh c unajua mtu ukiwa katika harakati za kutafuta mchumba unatupa huku na huku, nikaamua nimpe hi then nikaomba namba ili tuwe tunawasiliana....
    Baada ya muda mawasiliano yalikuwa makubwa sana tena sana akawa anakuja hadi ofsn kwangu......
    Kilichofanya nilete hii mada hapa ndan ni siku huyu binti alipokuja ndan kwangu.....
    Ili ajionyeshe kuwa yeye ni salama i mean kashapima akaja na cheti cha angaza akiwa amekipiga picha kikiwa kwenye cm yake.....hilo suala linitia hofu kidogo kwani sikuamini kama ni kweli au danganya toto...

    Siku hyo alidai anataman kuwa na mm kimapenz...., nashukuru nimepewa uwezo wa kuvumilia nilimkatalia nikamwambia nashukuru yeye kapima bt hapaswi kuniamni mimi nikamuomba asubuhi yake tukapime ili wote tuwe na uhakika tufaidi penz letu kwa raha....
    Huwezi amin asubuhi nikachukua tax nikambeba ili tukapime, tulipofika sehemu husika nikaomba nikamuone doctor then nitamuita......eeeeeeeeeh niliporudi sikumkuta na simu yangu hakupokea tena na sijawah kumuona tena....
    Vijana tuweni makini hii ni zaidi ya hatari kama watu wamefikia kuforge vyeti vya angaza...????







Previous Post Next Post