UKOSEFU WA GAS YAKWAMISHA CHANJO YA KUHARA NA KICHOMI KWA WATOTO

Na. Mwanja Ibadi Ruangwa

UKOSEFU wa gesi kwa baadhi ya zahanati  na vituo vya afya wilaya Ruangwa mkoani Lindi  ni moja ya changamoto zinazochangia kukwamisha zoezi la utoaji chanjo ya watoto ya  kuzuia ugonjwa wa kuharisha na kichomi( PCV na Rorotavirus) inayoendelea hapa nchini.

hayo yameelezwa na mratibu wa chanjo wilaya  hiyo Joyse Mchopa  wakati alipokuwa anazungumza na mwaandishi wa habari aliyetembelea wilayani humo jana.

mchopa  alisema kuwa zoezi la chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kuhara na kichomi inayotolewa  kwa watoto wenye umri wa  wiki sita chanjo ya kwanza  na wiki 10 chanjo ya pili  na ya tatu wiki 14 imekwama kwa baadhi ya vituo kutokana na kukosekana kwa mitungi ya gasi kwa ajili ya majokofu ya kuhifadhia dawa.

alisema chanjo hiyo inawalenga watoto wenye umri wa chini ya mwaka mmoja  ambao hawajapata  chanjo  kabisa  na kwamba watoto hao wataepuka kupata hatari ya magonjwa.

alisema lengo la chanjo hiyo ni kuwawezesha  watoto kupata kinga ya mwili ambayo itasaidia  kupambana na  maradhi  mbalimbali  ambayo   ni kikwazo kwa ukuaji na  maisha yao kwa ujumla.

mchopa alisema chanjo hizo zna mkinga  mtoto  kuambukizwa  na magonjwa  zaidi ya tisa ambayo ni kifua kikuuu, kupooza, surua, donda koo, kichomi , homa ya manjano, kifaduro, kuharisha,pepopunda, polio na uti wa mgongo,

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Rebeun Mfune alikiri kuwepo kwa tatitzo la ukosefu wa gesi kwa baadhi ya zahanati na vituo vya afya.

mfune alisema kuwa halmashauri imeanza kulifanyia kazi suala hilo ili kuhakikisha kuwa watoto wanaostahili kupata huduma wanapata kwa wakati.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post