MVUA YADORORESHA SIKUKUU YA PASAKA–LINDI

DSC04562POLISI MESS, MJINI LINDIDSC04561Baadhi ya Watoto wakisherehekea sikukuu ya Pasaka mara baada ya Mvua Kukatika.
Leo ikiwa ni siku ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka kwa waumini wa dini ya Kiikristo, sikukuu hiyo imeingia dosari kwa wale wanaopenda kutembelea sehemumbali mbali za miji, Mvua kubwa iliyonyesha mjini hapa imefanya watoto na watu wazima kukaa majumbani mwao na kusherehekea sikukuu hiyo kwani haikuwa kazi rahisi kutoka na mvua hiyo iliyo dumu kwa masaa kadhaa na kutengeneza ma bwawa ya muda. kama ilivyo sehemu nyingi suala la miundombinu ni tatizo kwani maji yanashindwa kupita katika mifereji au sehemu zingine mifereji kuzidiwa na uwingi wa maji hayo.
DSC04560Hapa paligeuka bwawa la muda kwani maji hutuama kwa wingi. Hushindwa huingia kwenye daraja lililopo eneo hilo kwa kuwa daraja hilo liko juu zaidi na hakuna mfereji pembezoni mwa barabara hiyo. Nyumba za eneo hili ziko hatarini kubomoka kwa kuliwa na Maji, ukizingatia ni za siku nyingi na zimesha choka. Mamlaka husika wanaliona jambo hili kila msimu wa mvua lakini Jitihada za kutatua suala hili hakuna.
Previous Post Next Post