NIGERIA WAPEWA AHADI YA NGONO BURE WIKI MOJA NA CHAMA CHA MACHANGUDOA NCHINI KWAO IKIWA WATABEBA UBINGWA WA AFRIKA

Machangudoa nchini Nigeria wamesema wamefurahia sana ushindi wa Super Eagles dhidi ya Ethiopia katika mashindano ya AFCON yanayoendelea nchini Afrika ya Kusini.
Machangudoa hao kupitia chama chao cha aegis of Nigeria Association of Prostitutes wamewasisitiza wachezaji wa timu ya taifa ya Nigeria kujitahidi na kushinda kombe hilo. Katika taarifa iliyotolewa na kusainiwa na katibu mkuu wa chama hicho Jessica Elvis.
“Tunapenda kuwapongeza wachezaji na makocha wa timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles kwa kufuzu kuingia robo fainali raundi inayofuatia ya mashindano. Tungependa kuwapa uhakika wa sapoti yetu ili waweze kuleta ushindi nyumbani.
"Katika kuonyesha sapoti yetu kwa timu ya taifa, tutatoa ofa ya wiki moja ya mapenzi bure kwa Super Eagles ikiwa watashinda ubingwa wa Afrika," alisema katibu mkuu wa chama hicho cha machagundoa.
Inasemekana baadhi ya wanachama wa chama hicho wapo nchini South Africa wakiisapoti timu hiyo kwenye mashindano ya AFCON.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post