Chelsea mambo magumu yalala tena

Glen Johnson amefanikiwa kuipatia ushindi Liverpool kwa bao la dakika za mwisho wakati Chelsea ilipolala kwa mabao mabao 2-1 katika uwanja wao wa Stamford Bridge.

image

Liverpool walikuwa wa kwanza kupata bao katika kipindi cha kwanza lililofungwa na Maxi Rodriguez katika dakika ya 33 baada ya gonga ya hapa na pale ya Craig Bellamy na Luis Suarez.

Daniel Sturridge aliyeingia kipindi cha pili aliisawazishia Chelsea kutokana na juhudi kubwa iliyooneshwa na Florent Malouda katika dakika ya 55.

Branislav Ivanovic nusura aipatie Chelsea bao la pili alipopiga kichwa lakini mpira huo ukaokolewa, lakini alikuwa mlinzi wa upande wa kulia Johnson aliyeihakikishia pointi tatu muhimu Liverpoo kutokana na jitahada zake binafsi alipokokota mpira upande wa kushoto na kuwapita walinzi wa Chelsea kama anafanya mazoezi na kupachika bao safi la pili.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post