Klabu ya ligi kuu ya Uingereza Manchester United leo wamethibitisha kumsajili winga Ahley Young kutoka Aston Villa kwa mkataba wa miaka mitano kwa kitita cha pauni za Uingereza milioni £17m., baada ya kufaulu vipimo vya afya jana jioni. Young - ambaye hivi majuzi aliifungia England wakati walipotoka sare ya magoli 2-2 na Switzerland -amechezea timu yake ya taifa mara 15.
Young anakuwa mchezaji wapili kuthibitishwa kusajiliwa na Man United bada ya Phil Jones wiki iliyopita.
Tags
Usajili Barani Ulaya