SIMBA SC YAIFUMUA BULA HURUMA TOTO AFRIKA YA MWANZA 3-0

Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba iliyokuwa mwenyeji wa Toto Africans ya Mwanza umemalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa goli tatu kwa bila.
Mzamiru Yassin
Ushindi wa Simba umepatikana kupitia Mzamiru Yassin akifunga magoli katika dakika ya 42 na 74, na goli lingine likifungwa na mchezaji raia wa Burundi, Laudit Mavugo katika dakika ya 51.

Kwa matokeo hayo Simba imefikisha alama 29 ikiongoza msimamo wa VPL, imecheza michezo 11 na ikiwa na mchezo mmoja mkononi, nafasi ya pili ikishikiliwa na Yanga yenye alama 21 huku Toto Africans ikisalia mkiani na alama nane katika michezo 12.

Mchezo unaofuatia kwa Simba ni Jumamosi ya Oktoba, 29 dhidi ya Mwadui ya Shinyanga.

MSIMAMO WA LIGI YA VODACOM HIVI SASA
VPL msimamo

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post