Unknown Unknown Author
Title: ROMA NA STAMINA HIVI NDIVYO WALIVYOICHA FIESTA YA MWAKA HUU
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Imetimia mikoa 14 ambayo team ya Fiesta imezunguka na kutoa burudani ya uhakika na kutoa fursa kibao katika mikoa hiyo husika. Kila m...
Imetimia mikoa 14 ambayo team ya Fiesta imezunguka na kutoa burudani ya uhakika na kutoa fursa kibao katika mikoa hiyo husika.
 Roma Mkatoliki na Stamina,
Kila mmoja ana mtazamo wake kuhusiana na Fiesta ya mwaka huu. Lindiyetu.com imepiga story na wasanii wawili wa Hiphop Roma Mkatoliki na Stamina, na wao wametupa tathmini yao kwa mtazamo wao walivyoiona Fiesta ya mwaka huu.

Stamina

“Cha kwanza naomba niwapongeze Tigo pamoja na Clouds, wamejipanga, kuna mabadiliko mengi sana kwenye Fiesta hii na Fiesta zilizopita, kuanzia produntion mpaka kwa wasanii wenyewe ufanyaji wao wa show, umekuwa tofauti sana watu wamejipanga, nilikuwa napenda sana idea za show zilizokuwa zinatokea watu kama Benpol, Mr Blue Byser na wengineo. Kiukweli kama inavyojulikana hamna tamasha kubwa Tanzania kama Fiesta, lakini nimeonyesha kabisa kuwa namimi nashukuru kuwepo katika msimu mwingine wa Fiesta.”

Roma Mkatoliki
“It went good, imekuwa kubwa sana, nadhani Clouds huwa wanajaribu kufanya kila mwaka Fiesta wanayofanya kuwa kubwa kuliko ya mwaka uliopita, na siku zote ukitaka kufanikiwa katika maisha hakikisha unafanya kitu bora kuliko kilichopita. Hata mimi kwenye muziki wangu nahakikisha ngoma ninayotoa 2005 ni kali kuliko ya 2004. Fiesta 2016 imekuwa more professional, kikubwa ambacho nimejifunza na nime enjoy ni pale bosi aliposema tubadilishe show. Me ni Roma, naimba miaka 7 sasa kila mtu anajua nyimbo zangu, na kila mtu anajua nikipanda jukwaani ni lazima niimbe Mathematics na nyinginezo, kinachojiri ni kutoa kitu cha ziada ili mtu asisite kutoa elf 10 yake tena mwaka ujao.”

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top