Unknown Unknown Author
Title: BABU TALE AIKACHA SHEREHE YA NDOA YA MSANII TUNDA MAN
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Siku ya Jana msanii Captain Tundaman kutoka Tiptop Connection iliyopo chini ya meneja Babu Tale amefanikiwa kutimiza nusu ya dini kwa i...
Siku ya Jana msanii Captain Tundaman kutoka Tiptop Connection iliyopo chini ya meneja Babu Tale amefanikiwa kutimiza nusu ya dini kwa imani ya dini yake (Kufunga ndoa) huko mjini Morogoro.
Ndoa ya Tunda Man
Kitu ambacho ni cha kustaajabisha na kilichozua mjadala katika siku hii muhimu kwa msanii Tundaman ni kwamba meneja wake Babu Tale hakuweza kuhudhuria katika tukio hilo muhimu la msanii wake. Ukizingatia timu nzima ya wasanii wa Tiptop Connection walikuwepo eneo la tukio.

Kitu ambacho kimewashangaza wengi na kuzua maswali kibao ya sintofahamu huku wakijadili kuwa endapo ingekuwa ni shughuli ya msanii Diamond Platnumz (ambaye ni anammeneji pia) je! meneja huyo angeshindwa kuhudhuria?
Ndoa ya Tunda Man
Lindiyetu.com imeona nivyema kufikisha madukuduku ya wadau, wewe kama mpenzi na mmoja wa wafuatiliaji wa tasnia ya burudani una kipi cha kusema juu ya hili? 

Tu-shee mawazo hapa chini kwenye uwanja wa comments.
****************

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top