Siku ya Jana msanii Captain Tundaman kutoka Tiptop Connection iliyopo chini ya meneja Babu Tale amefanikiwa kutimiza nusu ya dini kwa imani ya dini yake (Kufunga ndoa) huko mjini Morogoro.
Kitu ambacho ni cha kustaajabisha na kilichozua mjadala katika siku hii muhimu kwa msanii Tundaman ni kwamba meneja wake Babu Tale hakuweza kuhudhuria katika tukio hilo muhimu la msanii wake. Ukizingatia timu nzima ya wasanii wa Tiptop Connection walikuwepo eneo la tukio.
Kitu ambacho kimewashangaza wengi na kuzua maswali kibao ya sintofahamu huku wakijadili kuwa endapo ingekuwa ni shughuli ya msanii Diamond Platnumz (ambaye ni anammeneji pia) je! meneja huyo angeshindwa kuhudhuria?
Lindiyetu.com imeona nivyema kufikisha madukuduku ya wadau, wewe kama mpenzi na mmoja wa wafuatiliaji wa tasnia ya burudani una kipi cha kusema juu ya hili?
Kitu ambacho ni cha kustaajabisha na kilichozua mjadala katika siku hii muhimu kwa msanii Tundaman ni kwamba meneja wake Babu Tale hakuweza kuhudhuria katika tukio hilo muhimu la msanii wake. Ukizingatia timu nzima ya wasanii wa Tiptop Connection walikuwepo eneo la tukio.
Kitu ambacho kimewashangaza wengi na kuzua maswali kibao ya sintofahamu huku wakijadili kuwa endapo ingekuwa ni shughuli ya msanii Diamond Platnumz (ambaye ni anammeneji pia) je! meneja huyo angeshindwa kuhudhuria?
Lindiyetu.com imeona nivyema kufikisha madukuduku ya wadau, wewe kama mpenzi na mmoja wa wafuatiliaji wa tasnia ya burudani una kipi cha kusema juu ya hili?
Tu-shee mawazo hapa chini kwenye uwanja wa comments.
****************
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.