MAN UNITED YAINYUKA ZORYA LUHANSK EUROPA LEAGE

MAN UNITED wameifunga Zorya Luhansk ya Ukraine 1-0 katika Mechi yao ya pili ya Kundi A la UEFA EUROPA LIGI.
Man United
Ushindi huu umeiweka Man United kwenye Reli baada ya kupoteza Mechi yao ya kwanza ya Kundi A huko Rotterdam walipofungwa na Feyenoord 1-0.

Bao la ushindi la Man United lilifungwa Dakika ya 69 kwa Kichwa na Zlatan Ibrahimovic kufuatia Krosi ya Fulbeki Fosu-Mensah kuunganishwa fyongo na Wayne Rooney na Mpira kudunda juu na Ibrahimovi kuumalizia.
Man United
Bao hilo lilikuja Dakika 2 tu baada ya Rooney kuingizwa Uwanjani kumbadili Jesse Lingard.

Kwenye Mechi nyingine ya Kundi A iliyochezwa huko Uturuki, Fenerbahce iliitungua Feyenoord 1-0.

Mechi inayofuata kwa Man United ni Oktoba 20 na Fenerbahce Uwanjani Old Trafford.

VIKOSI: Man United: Romero; Fosu-Mensah [Martial, 74’], Bailly, Smalling, Rojo; Fellaini, Pogba; Lingard [Rooney, 67’], Mata [Young, 74’], Rashford; Ibrahimovic.
Akiba: Johnstone, Carrick, Schneiderlin, Young, Martial, Memphis,Rooney

Zorya Luhansk: Shevchenko; Sivakov, Chaykovsky, Kamenyuka, Petriak, Kulach [Melo, 60’], Forster, Karavaev, Ljubenovic [Lipartia. 76’], Grechyshkin, Sobol
Akiba: Chuvayev, Sukhotsky, Gordiyenko, Lipartia, Paulinho, Opanassenko, Chercher

REFA: O Greinfeld (Israel)

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post