WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI WAWATAKA WANANCHI KUPENDA BIDHAA ZA NDANI

Viwanda Nane nane 2016-1
Ndg: Odilo Majengo Mkurugenzi wa Uhamasishaji Biashara na Masoko wizara ya Viwanda na Uwekezaji Akizungumza na waandishi wa habari katika Banda la wizara hiyo lililopo Viwanja vya Nane nane Ngongo Mkoani Lindi, Odilo amewataka wananchi kwa ujumla kutembelea Banda hilo iliwaweze kujionea na kufahamu uhusiano wa Kilimo na azma ya Tanzania ya Viwanda kama kaulimbiu ya Serikali ya awamu ya Tano inavyoeleza. Aidha amewataka wakulima kuuza mazao yaliyosindikwa ilikuweza kupanua masoko.
Viwanda Nane nane 2016-2
Ndg: Edwin N Rutageruka mkurugenzi wa Tantrade Tanzania Akizungumza na waandishi wa habari katika Banda la wizara hiyo lililopo Viwanja vya Nane nane Ngongo Mkoani Lindi, Aidha Rutageruka ameeleza kuwa moja ya shabaha ya wizara ni kuwaunganisha wazalishaji na wanunuzi ilikufanikisha bidhaa hiyo kuuzwa katika soko la ndani na nje kwa ujumla. pia amewataka watanzania kupenda kununua bidhaa za ndani kuliko kutegemea sana bidhaa zinazotoka nje ili kukuza uchumi na kuongeza kipato cha wakulima nchini.
Viwanda Nane nane 2016-3
Moja ya Zana za Kilimo zilizo Buniwa na kiwanda cha Sido Lindi. 
Viwanda Nane nane 2016-4
Moja ya Zana za Kilimo zilizo Buniwa na kiwanda cha Sido Lindi.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post