TANZIA: MSANII WA BONGO FLEVA AFARIKI DUNIA, YASEMEKANA ALIKUWA KWENYETUKIO LA KIJAMBAZI

lindiyetu logo 3
Msanii na mtunzi wa nyimbo za bongo fleva, Hamid Hafidhi maarufu kama Ude Ude amefariki dunia akiwa mkoani Tanga.



Akiripoti kuhusu tukio hilo kwenye kipindi cha Papaso cha TBC, Baghdad amesema kuwa chanzo cha kifo cha marehemu bado hakijawekwa hadharani lakini taarifa za mwanzo zinaeleza kuwa msanii huyo alifikwa na mauti yeye na rafiki yake wakiwa katika tukio linalosadikiwa kuwa ni la kijambazi na inaelezwa kuwa marehemu na wenzake wamekuwa wakijihusisha na matukio hayo mara kwa mara kwa kivuli cha heshima waliyo nayo kwenye jamii.
Ude Ude na Iku
Marehemu Ude Ude na rafiki yake Iku ambao wote wamefariki kwenye tukio hilo enzi za uhai wao

Marehemu Ude Ude alijipatia umaarufu kwenye muziki wa bongo fleva kwa umahiri wake wa kuwatungia nyimbo wasanii ambapo nyimbo alizozitunga ni pamoja na Wangu na Yahaya za Lady Jay dee. Wimbo wake ulioweza ku hit ni Ngoma Inogile waweza icheki hapo chini.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post