Kama unakumbuka Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) lilitangaza kumfungia msanii wa bongo fleva Shilole kutokana na sababu za kinidhamu hapo mwaka 2015, lakini msanii huyo amekuwa akionekana kuendelea na shughuli za sanaa tofauti na agizo hilo.
Alipoulizwa kuhusina na Suala hilo kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio katibu wa BASATA,Bw. Godfrey L. Mngereza amedai kuwa Shilole alifuata taratibu zote alizotakiwa na baadaye kukata rufaa kwenye ngazi kubwa zaidi na adhabu yake ikaisha.
“Unajua sio kila kitu baraza tunatangaza,suala la Shilole ni kwamba alifuata taratibu na kwenda ngazi zingine na kukata rufaa kwa hiyo ilifikia huko na kumalizwa” alisema katibu huyo wa BASATA ambapo hivi karibuni wametangaza kumfungia msanii wa Hip Hop Nay wa Mitego.
Alipoulizwa kuhusina na Suala hilo kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio katibu wa BASATA,Bw. Godfrey L. Mngereza amedai kuwa Shilole alifuata taratibu zote alizotakiwa na baadaye kukata rufaa kwenye ngazi kubwa zaidi na adhabu yake ikaisha.
“Unajua sio kila kitu baraza tunatangaza,suala la Shilole ni kwamba alifuata taratibu na kwenda ngazi zingine na kukata rufaa kwa hiyo ilifikia huko na kumalizwa” alisema katibu huyo wa BASATA ambapo hivi karibuni wametangaza kumfungia msanii wa Hip Hop Nay wa Mitego.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.