NAY WA MITEGO AKIFUATA NYAYO ZA SHILOLE ANAWEZA KURUDI KWENYE GAME, BASATA WAFUNGUKA

Kama unakumbuka Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) lilitangaza kumfungia msanii wa bongo fleva Shilole kutokana na sababu za kinidhamu hapo mwaka 2015, lakini msanii huyo amekuwa akionekana kuendelea na shughuli za sanaa tofauti na agizo hilo.
Shilole
Alipoulizwa kuhusina na Suala hilo kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio katibu wa BASATA,Bw. Godfrey L. Mngereza amedai kuwa Shilole alifuata taratibu zote alizotakiwa na baadaye kukata rufaa kwenye ngazi kubwa zaidi na adhabu yake ikaisha.
Nay wa Mitego
“Unajua sio kila kitu baraza tunatangaza,suala la Shilole ni kwamba alifuata taratibu na kwenda ngazi zingine na kukata rufaa kwa hiyo ilifikia huko na kumalizwa” alisema katibu huyo wa BASATA ambapo hivi karibuni wametangaza kumfungia msanii wa Hip Hop Nay wa Mitego.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post