WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA APIGA MARUFUKU UVUTAJI WA SHISHA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku uvutaji wa Shisha.
Shisha
Ameliagiza jeshi la polisi kufanya kazi kuhakikisha ulevi huo unapotea kabisa ili kuwalinda vijana wanaoutumia zaidi.

Ametoa agizo hilo kwenye hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na madhehebu ya Shia nchini mwishoni mwa wiki. Limekuja siku moja tu baada ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda naye kupiga marufuku uvutaji wa kilevi hicho pamoja na vitendo vya ushoga na uvutaji sigara hadharani.

Mheshimiwa Majaliwa alidai kuwa Shisha ni kilevi ambacho huchanganywa na vitu vingine vikiwemo viroba na pombe zingine.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post