NIJUZE NIJUZE Author
Title: RPC CUP- MNAZI MMOJA YAICHAPA MBAJA 2-0
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya Kata ya Mnazi Mmoja imeifunga timu ya Kata ya Mbanja kwa jumla ya magoli 2-0 katika Mashindano ya RPC - CUP yanayoendelea katika Uw...
Timu ya Kata ya Mnazi Mmoja imeifunga timu ya Kata ya Mbanja kwa jumla ya magoli 2-0 katika Mashindano ya RPC - CUP yanayoendelea katika Uwanja wa Ilulu ndani ya Manispaa ya Lindi.
Ni Abdallah Ismail a.k.a Baloteli ndiye aliyeibuka Shujaa wa Mchezo huo baada ya Kuifungia Timu yake ya Mnazi mmoja magoli yote mawili ambayo yalipatikana katika dakika ya 38 na 50 ya Mchezo huo. 

Hata hivyo Timu hiyo ya Mnazi mmoja walionekana kuidhibiti vilivyo wapinzani wao na kama safu ya Ushambuliaji ingekuwa makini ingeweza kuibuka na ushindi mmnono wa Magoli mengi zaidi.
Mnamo dakika ya 48 Timu ya Kata ya Mbanja waliweza kumpoteza Beki wao ambaye alivalia jezi namba 10 baada ya Kuzawadiwa kadi nyekundu mara baada ya Kuunawa Mpira kwa makusudi pale alipokuwa akitorokwa na Mshambuliaji Machachari wa Timu pinzani.

Hadi Mwisho wa Mchezo Mnazi mmoja waliibuka washindi wa Mechi hiyo kwa Jumla ya magoli 2-0.
TIMU YA KATA YA MMNAZI MMOJA
KIKOSI CHA KWANZA CHA TIMU YA KATA YA MMNAZI MMOJA DHIDI YA KATA YA MBANJA
TIMU YA KATA YA MBANJA
KIKOSI CHA KWANZA CHA TIMU YA KATA YA MBANJA DHIDI YA KATA YA MMNAZI MMOJA

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top