MBUNGE WA MCHINGA MH. BOBAL AITAKA SERIKALI KUTOA VIBALI VYA UINGIZAJI SUKARI KUEPUKA SUKARI ISIYO SALAMA

Mh. Hamidu Bobali
Kutokana na Uhaba wa sukari nchini Mbunge wa mchinga Mh. Hamidu Bobali ameitaka serikali ya awamu ya Tano ya Mh. Rais Magufuli kutoa kibali ili waweze kuingiza Sukari kwa njia halali.

Akizungumza na Lindiyetu.com Mh. Bobali amesema nchi itakua na upungufu wa sukari wa tani laki mbili kuanzia Tarehe 15 mwezi wa 4.


Amesema kuzuia uingizwaji wa Sukari nchini kunaweza leta Matatizo kwani sukari hiyo inaweza kuingizwa kwa njia za Panya na kusababisha kuingizwa sukari isiyo salama kwakuwa haitakuwa imethibitishwa na Mamlaka ya Chakula TFDA.

SIKILIZA SAUTI YA MAHOJIANO NA MWANDISHI WETU
Previous Post Next Post