MBOWE AKOSOA UTUMBUAJI WA MAJIPU SERIKALI YA AWAMU YA TANO, ASHAURI JAMBO HILI

Freeman Mbowe
Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe ameweza kuongea na viongozi wa Chama Mkoa wa Dar es Salaam, Madiwani pamoja na Wabunge wa mkoa huo kuelezea hali ya kisiasa jijini Dar es Salaam na nchi kwa ujumla. 

Katika kikao hicho Mwenyekiti wa Chama cha Chadema ameweza kugusia jinsi Majipu yanavyotumbuliwa na Serikali ya Rais Magufuli, amesema ni kweli wapo ambao wanamakosa hayo lakini kunawengine wanatumbuliwa kwakuwa tu wanahisiwa au wanaonekana wana uchadema.

Pia Mbowe amebainisha kuwa nivyema watumbuaji wakaeleza jamii ni nini watumbuliwaji wamefanya makosa yapi na hatua stahiki za kisheria zikachukuliwa juu yao.


Unaweza Tazama Video hii hapa Chini:
Previous Post Next Post