Maisha ya watu wengi maarufu yana mapito mbalimbali yenye furaha na huzuni.
Kwa upande wake msanii anae ipeperusha vyema Bendera ya Tanzania Nasib Abdul maarufu kama Diamond Plutnumz ameripotwa kutoka kimapezi na warembo wengi mashuri akiwemo Wema Sepetu, Jokate Mwegelo, Jackline Wolper, Pennie na wengine wengi.
Katika warembo hao kila mmoja ana mazuri na mabaya yake, akizungumza katika kipindi cha Leo Tena kinachorushwa na Clouds FM wakati wakitambulisha wimbo mpya wa msanii Harmonize aliomshirikisha Diamond uitwao Bado, Diamond alifunguka juu ya mwanamke ambaye hawezi kumsahau.
Akizungumzia suala hilo Diamond alisema Harmonize alimuuliza kama aliwahi kuumizwa na hawezi kusahau, Diamond akafunguka na kusema kuwa hawezi kumsahau mpenzi wake aliyempenda sana anae tambulika kwa jina la Sarah Sadiki, huku akisisitiza kuwa inaweza isiwe kimapenzi ila huwa anamkumbuka tu.