
Sababu ya amri hiyo ni kutokana na mashtaka yaliyokuwa yakimkabili ya kutumia fedha za umma kinyume na utaratibu akiwa madarakani ili kufanya upelelezi kwa takriban watu 150 maarufu nchini mwake.
Miongoni mwa waliodaiwa kudhurika na upelelezi huo uliofanyika kinyume cha sheria ni pamoja na wafanyabiashara, wanasiasa, wanasheria, madaktari pamoja na wanachama wa umoja wanaharakati wafanyabiashara.
Taarifa zinasema Mahakama imefi kia uamuzi wa kumkamata Martinelli baada ya kushindwa kutokea mahakamani mwanzoni mwa mwezi huu, kwa ajili ya shauri la kwanza.
Kutokujitokeza kwake mahakamani kunasemekana ni kwa makusudi kwa kuwa anaishi mji wa karibu na mahakama hiyo jimbo la Miami.
Tags
HABARI KIMATAIFA