LICHA YA MFULULUZI WA AJALI MBAYA MWEZI MARCH/APRIL. TAKWIMU ZAONESHA KUPUNGUA KWA AJALI ZA BARABARANI MWAKA 2015

Licha ya mfululizo wa ajali mbaya zilizotokea kati ya mwezi March na April Mwaka huu lakini Takwimu zinaonyesha kupungua kwa kiwango kikubwa kwa ajali za barabara kwa mwaka 2015 ukilinganisha na Mwaka 2014 katika kipindi kama hicho.
Ajali
Akisoma bajeti wa Wizara ya Mambo ya Ndani leo Bungeni Waziri wa Mambo ya ndani Mh. Mathius Chikawe amesema Takwimu zinaonyesha kuwa 2718 ya ajali zote ukilinganisha na ajali 6050 zilizotokea katika kipindi kama hicho kwa mwaka jana.

Mh. Chikawe amesema ili kudhibiti na kupunguza zaidi ajali za barabarani serikali imechukua hatua kadhaa ili kukomesha matukio hayo ambayo kwa mwaka huu pekee watu 2883 walipoteza maisha wakati watu 9370 wamejeruhiwa.
Previous Post Next Post