NI MAJONZI KATIKA SOKA TENA: MCHA KHAMIS AFARIKI DUNIA

Khamis Mcha ‘Vialli’
Kiungo wa Azam FC na Taifa Stars Khamis Mcha ‘Vialli’ (pichani) amefiwa na baba yake mzazi, Mcha Khamis, mchezaji wa zamani wa KMKM.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Zanzibar, Mcha Khamis amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.

Baba huyo wa kiungo wa Azam FC na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars Khamis Mcha ‘Vialli’ amefariki duniani mjini Dar es Salaam ambako alikuwa anapatiwa matibabu.

Enzi za uhai wake, Mcha mkubwa alichezea klabu za KMKM na Miembeni pamoja na timu ya taifa ya Zanzibar. Pumzika kwa amani Mcha Khamis, ahadi yako imetimia.

Source:: BinZuberi

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post