Miili ya Wanafunzi sita na Mwalimu ikiwa tayari kwa kuagwa katika viwanja vya shule ya Msingi Kibirizi mkoani Kigoma . WATU wanane wakiwemo wanafunzi sita na mwalimu wa shule ya msingi kibirizi mmoja pamoja na mtu wa kawaida mkazi wa eneo la Bangwe mjini hapo walipoteza maisha hapo jana baada ya kupigwa na radi huku wanafunzi wengine 15 kujeruhiwa na radi hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Kanali Mstaafu Issa Machibya akisoma salamu za rambi rambi za mkoa wakati wa kuaga miili ya Wanafunzi na Waalimu waliopigwa na radi jana.
Katibu wa Bakwata mkoa wa Kigoma,Shekhe Moshi Guoguo akituma salamu za rambirambi kwa wafiwa.
Wanajeshi wa JWTZ wakiingiza miili ya marehemu katika viwanja vya shule ya msingi Kibirizi kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho.
Source:: Michuzi Media Group
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.