Unknown Unknown Author
Title: MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO WATISHIA KUGOMA IJUMAA KWA MADAI YA KUFANYIA UNYANYASAJI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mabasi ya Abiria yakiwa yamepaki stand Madereva wa vyombo mbali mbali vya moto nchini Tanzania, wanakusudia kushiriki mgomo wa nchi n...
mabasi yaendayo mkoani
Mabasi ya Abiria yakiwa yamepaki stand

Madereva wa vyombo mbali mbali vya moto nchini Tanzania, wanakusudia kushiriki mgomo wa nchi nzima siku ya Ijumaa wiki hii, kuishinikiza serikali kuondoa kero mbali mbali zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa ajira za uhakika pamoja na agizo la kutaka madereva hao waende kusoma kila wanapotaka kuhuisha leseni zao za udereva.

Wakizungumza na Lindiyetu.com kupitia Katibu wa Muungano wa vyama vya Madereva Bw. Rashid Saleh, madereva hao wamesema kuwa suala la kurudia kusoma ni aina nyingine ya unyanyasaji kwa maelfu ya madereva nchini, ambao kwa kipindi kirefu wamekuwa hawana mfumo mzuri wa ajira licha ya kutupiwa lawama kibao kuwa wao ndio chanzo cha ongezeko la ajali nchini.

Katibu huyo wa Muungano wa Vyama vya Madereva ameitaja kero nyingine kuwa ni hatua ya Chuo cha Taifa cha Usafirishaji NIT kutamka hadharani kuwa vyeti walivyonavyo madereva hao sio halali na kwamba Ijumaa wiki hii wanakusudia kukutana na Waziri wa Kazi na Ajira kwa ajili ya kuzungumzia kero hizo kwa lengo la kuepusha kutokea kwa mgomo huo.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top