Unknown Unknown Author
Title: MAAFISA ARDHI DAR ES SALAAM WAPEWA SIKU 30 KUTATUA KERO ZA WANANCHI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi WILLIAM LUKUVI Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi WILLIAM LUKUVI ametoa sik...
WILLIAM LUKUVI
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi WILLIAM LUKUVI

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi WILLIAM LUKUVI ametoa siku 30 kwa maafisa wa ardhi na watendaji mkoani DSM kuhakikisha wanashughulikia na kutafuta ufumbuzi wa kero mbalimbali za ardhi jijini humo.

Akizungumza na maafisa watendaji kutoka Manispaa za TEMEKE, ILALA na KINONDONI Waziri LUKUVI amesema Manispaa ya KINONDONI inaongoza katika migogoro ya ardhi ambapo amesema wakazi wake wanakabiliwa na shida kubwa hasa katika upimaji wa viwanja.

Waziri LUKUVI amewataka watendaji wa sekta hiyo kushiriki kikamilifu kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi hususani kwenye sekta hiyo.

Katika kukabiliana na tatizo hilo, amesema serikali inatarajia kuanza kutumia mfumo mpya wa usimamizi wa rasilimali ardhi unaojulikana kama Land Management System utakaotumika katika usimamizi, upimaji, upangaji, utoaji wa hati pamoja na kufichua udanganyifu unaofanywa na baadhi ya maafisa wa wizara hiyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top