Unknown Unknown Author
Title: AUNT EZEKIEL "MAMA KIJACHO" AWAUMBUA WAIGIZAJI WA BONGO MOVIES, HICHI NDICHO ALICHOKISEMA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Staa mrembo wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel ‘Mama Kijacho’ amesema baadhi ya wasanii wa bongo movies hawajitambui ndio maana kazi zao nyingi ...
Staa mrembo wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel ‘Mama Kijacho’ amesema baadhi ya wasanii wa bongo movies hawajitambui ndio maana kazi zao nyingi hazina mvuto  badala yake nguvu nyingi wameelekeza kubuni skendo wakitarajia ndio zitawatoa kisanaa.
Aunty Ezekiel
Alisema wasanii wengi wanatumia muda mwingi kutafakari jinsi ya kutengeneza skendo ili watume kwenye mitandao na kuandikwa kwenye magazeti lakini hawana ubunifu  wa kutengeneza filamu zenye ushawishi kwenye jamii.

Aunt ambae kwenye filamu ya Chozi la Wanjaa amecheza kama mke wa Dude alisema kwamba endapo wasanii wanaofanya mchezo huo hawata badilika ni ukweli usiopingika  kwamba soko la filamu  inchni litaendelea kudumaa kama ilivyo sasa.

Ni ukweli kwamba baadhi ya wasanii wa filamu hawajitambui kwani akili yao wameelekeza kwenye kutengeneza skendo badala ya kubuni namna ya kuigiza filamu ambazo zinaweza kuwa na mvuto kwenye jamiiinayoziangalia kinyume na hapo tutaendelea kusaka wachawi wanaoua soko letu’- Aunt Ezekiel alilieza gazeti la Filamu

Mdau una maoni gani juu ya hoja hii ya wasanii kutengeneza skendo, je ni kweli? Msanii gani unahisi ndio kazi yake.

About Author

Advertisement

 
Top