Unknown Unknown Author
Title: KOCHA WA MANCHESTER UNITED KUBWAGA MANYANGA KAZI YA UKOCHA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Kocha mkuu wa klabu ya Manchester United Louis van Gaal ametangaza kustaafu kufundisha mpira pindi atakapomaliza mkataba wake wa kuitumikia...
Kocha mkuu wa klabu ya Manchester United Louis van Gaal ametangaza kustaafu kufundisha mpira pindi atakapomaliza mkataba wake wa kuitumikia klabu ya Manchester United.
Luis Van Gaal
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 63 ana mkataba wa kuifunza Manchester United hadi mwaka 2017.

Mholanzi huyo amesema hana mpango wa kuendelea na fani hiyo kwani muda wake uliobaki anahitaji kuwa na familia yake.
Van Gaal amewahi kuzifunza timu kadhaa barani Ulaya zikiwemo Barcelona, Bayern Munich na Ajax.

Akizungumza kwenye mahojiano yake na gazeti la daily Telegraph amesema umri wake umeenda na kwasasa anafikiri kustaafu ukocha baada ya kumaliza kibarua chake Old Trafford maana anahitaji kuwa karibu na mke wake, watoto wake na wajukuu zake.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top