Unknown Unknown Author
Title: MWINGINE MCHEZAJI WA SIMBA AFARIKI DUNIA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KIKOSI CHA SIMBA KILICHOING'OA ZAMALEK MWAKA 2003 Aliyekuwa kiungo nyota wa Simba, Christopher Alex Massawe, amefariki dunia. Ale...
KIKOSI CHA SIMBA 2003
KIKOSI CHA SIMBA KILICHOING'OA ZAMALEK MWAKA 2003

Aliyekuwa kiungo nyota wa Simba, Christopher Alex Massawe, amefariki dunia. Alex amefariki dunia akiwa mjini Dodoma ikiwa ni baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Dada wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Mama Maembe amesema Alex amefariki dunia jana saa 3 asubuhi. Tayari taratibu za mazishi zimeanza kufanywa na imeelezwa Alex atazikwa mjini humo.

Alijulikana kwa ubora wake katika ukabaji na kuichezesha timu. Lakini pia atakumbukwa kwa kuwa mchezaji aliyepiga penalti ya mwisho iliyoivua ubingwa Zamalek na kuipeleka Simba kucheza Kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika 2003, hatua ya makundi.

Christopher Alex Massawe
Christopher Alex Massawe enzi za uhai wake

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top