EPL:: MATOKEO YA MECHI YA MANCHESTER UNITED DHIDI YA LEICESTER CITY YAKO HAPA

Kumbukumbu za mchezo wao uliopita – Louis Van Gaal anasema ni kitu ambacho angependa kukisahau, wakiwa wanaongoza kwa magoli 3 mechi ikaishia kwa kufungwa 5-3 na Leicester City.
Manchester
Leo hii miezi takribani minne tangu mechi hiyo ya kwanza ya EPL kuchezwa, Leceister walisafiri mpaka jijini Manchester kwenda kucheza na Man United.

Mchezo huo uliopigwa katika dimba la Old Trafford umemalizika kwa Louis Van Gaal kuiongoza United kuweza kulipa kisasi kwa kuifunga Leceister kwa magoli 3-1.
Manchester
Magoli ya United yalifungwa na Van Persie, Radamel Falcao na moja la kujifunga kwa Leceister wenyewe.
Manchester
Mpaka timu hizo zinaenda mapumziko United walikuwa wanaongoza 3-0.
Manchester
Kipindi cha pili United walipunguza kasi na Leceister wakajaribu kufanya maajabu ya kusawazisha magoli na hata kupata ushindi kabisa lakini siku haikuwa yao – wakaishia kupata goli moja tu lilofungwa na Wasilewski.

VIKOSI:: MANCHESTER UNITED (4-1-2-1-2): De Gea 6; Valencia 7 (Mata 77, 6), Jones 6.5, Rojo 7, Shaw 7; Blind 7.5; Rooney 7, Januzaj 6.5; Di Maria 7; Van Persie 8 (McNair 68, 6), Falcao 7.5 (Wilson 80, 6)
Subs not used: Valdes, Smalling, Herrera, Fellaini
Goal: Van Persie 27, Falcao 32, Morgan OG 44
LEICESTER (4-4-2): Schwarzer 6; Simpson 5, Wasilewski 6.5, Morgan 5; De Laet 6; Vardy 5 (Cambiasso 46, 6), Drinkwater 5, King 6, Schlupp 5; Ulloa 5 (Nugent 62, 6), Kramaric 5 (Albrighton 62, 6.5)

1 Comments

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

  1. naona Manchester United inazidi kushine .....★

    ReplyDelete
Previous Post Next Post