Kikosi cha Kwanza cha Stand Worious kilichocheza dhidi ya Timu ya Magereza Fc Leo hii Kinachofundishwa na Ibrahim Ibrahim, Katika Ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Lindi katika Uwanja wa Ilulu
Kikosi cha Kwanza cha Magereza Fc kilichocheza dhidi ya Timu ya Stand Worious Leo hii, Katika Ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Lindi katika Uwanja wa Ilulu
Na. Mwandishi Wetu, Lindi
Ligi daraja la Tatu Mkoa wa Lindi Imeendelea Leo Hii kwa Kuzikutanisha Timu Mbili za Manispaa ya Lindi, Timu ya Stand Worious Yenye Maskani yake Stand Kuu ya Lindi na Timu ya Maafande wa Magereza Katika Dimba la Ilulu.
Ikiwa inapoint 2 kabla ya Ushindi wa Leo Timu ya Stand worious iliyokuwa inashika nafasi ya NNE ya Ligi hiyo Imeweza Kukwea nafasi Mbili Juu na Kuifikia Timu Inayoongoza Ligi kwa Kuwa na Point Sawa, Timu ya Marketi Fc zikiwa zote zina Point 5.
Hivyo na Kufanya Mchezo wa Mwisho kutabiriwa kuwa na Upinzani wa aina yake kwani Timu Hizo zitakutana zenyewe kwa zenyewe katika Kukamilisha Ratiba hiyo na Kufanya Timu zote kuwa na Kiu ya Kumaliza Ligi hiyo akiwa Mbabe. Timu ya Magereza Imebakia Mkiani mwa Ligi hiyo Kwa Kujikusanyia Point Moja Tu hadi sasa.
Katika Mchezo wa Leo Timu zilianza kwa Kushambuliana Kwa zamu Japo Pande zote mbili Washambuliaji wake hawakuwa Makini Kumalizia Mashambulizi yaliyokuwa yanafika langoni kwa Mwenzake.
Hadi Timu hizo Zinakwenda Mapumziko Hakuna Aliyeona Lango la Mwenzake. (Stand 0 - 0 Magereza)
Hadi Kipenga cha Mwisho Matokeo yalibakiwa kusomeka ( Stand 1 - 0 Magereza).
Hizi Ni baadhi ya Picha za matukiwa Kiwanjani:;
Kocha wa Magereza FC akitoa maelekezo wakati wa Mapumziko
Kocha wa Stand Worious akitoa maelekezo wakati wa Mapumziko
Mashabiki wa Mpira wakifuatilia kwa Makini Mchezo huo ambao Stand Worious waliibuka Washindi wa 1-0.
Heka Heka katika Lango la Magereza Fc....ambayo haikuzaa matunda
Wachezaji wa Stand Worious wakishangilia mara baada ya Mchezaji Andrea Kufunga Goli la Kwanza dhidi ya Magereza Fc
Wachezaji wa Stand Worious wakishangilia mara baada ya Mchezaji Andrea Kufunga Goli la Kwanza dhidi ya Magereza Fc
Mashabiki walifurika Ndani ya Uwanja wa Ilulu kushuhudia Mtanange Huo
Hii ni moja ya Mchomo Mkali ambao Golikipa wa Magereza aliuokoa......
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.