Ukiukaji wa haki za watoto unaendelea nchini Iraq, ambako watoto walemavu wanaendelea kutumiwa kufanya mashambulizi ya kigaidi, kwa imani kuwa wataweza kupona.Katika ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu nchini Iraq, wataalam wa haki za binadamu wameelezea pia kwa kina kuhusu kutumia watoto katika biashara ya ngono na kutengeneza picha na filamu za ngono, pamoja na vitendo vingine katili vinavyowalenga watoto wa kike.
Wataalam walioichangia ripoti hiyo wamesema matatizo mengi ya Iraq yalikuwepo hata kabla ya uvamizi wa kundi la kigaidi linalotaka kuweka dola la Uislamu wenye msimamo mkali, ISIL, mnamo mwaka 2014.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.