Unknown Unknown Author
Title: ALICHOKISEMA SHEDDY CLEVER JUU YA KUTOANDIKWA KWENYE VIDEO YA WIMBO WA "NITAMPATA WAPI" WA DIAMOND PLATNUMZ
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Producer wa hits mbili za Diamond Platnumz ‘Number One’ na ‘Ntampata Wapi’ alionekana kufurahia mafanikio ya Diamond kwenye tuzo za Channel...
Producer wa hits mbili za Diamond Platnumz ‘Number One’ na ‘Ntampata Wapi’ alionekana kufurahia mafanikio ya Diamond kwenye tuzo za Channel O, lakini kitu kimoja hakijakaa sawa moyoni mwake.
Sheddy Clever
Sheddy amesema ameshangazwa baada ya kutoona jina lake likiandikwa kwenye video ya ‘Ntampata Wapi’.

“Biashara kweli ni matangazo na nilitakiwa niandikwe kweli kwenye ile video, lakini sasa kwa sababu imeshapita na vitu vingi vimeshatokea na ukiangalia kwenye video international wanafanya hivyo ila mpaka sasa hivi najaribu kujiuliza sijapata jibu kamili kwanini wanafanya hivyo,” Sheddy ameiambia E-News ya EATV.

“Ukiangalia video za West Africa za akina Davido, Wizkid wengi producer wa audio wanakuwa hawaandikwi kwenye video. Sasa sijui wanafuta ule mfumo wa wenzetu, sifahamu.” Sheddy aliongeza

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top