Klabu ya Manchester inatarajiwa kuzikosa huduma za mlinzi wake wa kati raia wa Argentina Marcos Rojo mara baada ya kupata maumivu ya bega kwenye mchezo wa mahasimu wao wa mji mmoja klabu ya Manchester City.
Rojo alitolewa mapema kipindi cha pili na kuwekewa mtungi wa gesi ya oksijeni mara baada ya kupatwa na maumivu hayo ya bega kwenye mchezo huo.
"Ameumia bega, limetoka kwenye sehemu yake, hivyo huwezi kujua ni kwa muda gani atakua nje ya uwanja," Van Gaal alikiambia kituo cha televisheni cha Sky Sports cha nchini Uingereza. "Tuanatakiwa kusubiri mpaka kesho lakini kutokana na hali ya mambo ilivyo hataweza kucheza dhidi ya Crystal Palace."
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.