KIUNGO WA DYNAMO KIEV AITAMANI ARSENAL. HICHII NDICHO ALICHOKISEMA....!!!!

Younes Belhanda akipambana na wachezaji wa Arsenal

Na. Paul Manjale
Kiungo wa Dynamo Kiev Younes Belhanda(24) amefunguka kuwa ndoto na kiu yake ya kucheza ligi kuu ya England bado iko pale pale.Belhanda akifanya mazungumzo na gazeti la London 24 amesema ni hamu ya kila mchezaji kucheza hapo  na kujifunza mambo mengi nje na ndani ya uwanja.Belhanda ambaye ni mchezaji wa zamani wa klabu ya Montpellier ameongeza kuwa akipata ofa toka England basi chaguo lake la kwanza litakuwa ni kucheza katika klabu ya Arsenal kwa swahiba wake Olivier Giroud waliyecheza wote Ufaransa na kuipa taji klabu ya Montpellier.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post