BREAKING NEWZZ : TITO VILANONA KOCHA WA ZAMANI WA BARCELONA AFARIKI DUNIA

Goodbye Tito - a brave hero who created history at BarcelonaTITO VILANOVA AMEFARIKI DUNIA

Aliyekuwa kocha wa klabu ya Barcelona muhispania Fransesc `Tito' Vilanova(45) amefariki jioni ya leo katika hospitali moja mjini Barcelona kwa maradhi ya kansa.

Vilanova alianza kusumbuliwa na maradhi hayo November 2011 na kufanyiwa operation ya kwanza New York Marekani..

Vilanova alichukua mikoba ya kuifundisha Barcelona msimu wa 2012/2013 kutoka kwa kocha Pep Guardiola na kuweka rekodi mpya klabuni hapo baada ya kushinda mechi 18 kati ya 19 za mwanzo wa msimu na kufanikiwa kutwaa taji la La Liga kwa pointi 100.

Vilanova alizaliwa mwaka 1968 huko kijijini Bellcaire d' Emporda,alijiunga na kituo cha soka cha Barcelona mwaka 1984 mpaka 1989 lakini hakuweza kupata nafasi kikosi cha kwanza. Badala yake alitimkia Celta Vigo na kisha Mallorca mpaka hapo soka yake ilipokuja kukatwishwa na majeraha ya goti. 



Vilanova ameacha mke aitwaye Montse Chaure na watoto wawili huku mwanae mkubwa Adrian akiwa anajifunza soka La Masia.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post