Unknown Unknown Author
Title: WEST HAM KUMKATIA RUFAA CARROLL, MATA ADAI GUNDU LITAISHA!
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
WEST HAM imeijulisha FA nia yao ya kukata Rufaa kupinga Kadi Nyekundu ya Straika wao Andy Carroll aliyopewa Juzi Jumamosi walipoifunga Swans...

WEST HAM imeijulisha FA nia yao ya kukata Rufaa kupinga Kadi Nyekundu ya Straika wao Andy Carroll aliyopewa Juzi Jumamosi walipoifunga Swansea City.

Carroll alipewa Kadi Nyekundu na Refa Howard Webb baada kugongana na Beki wa Swansea, Chico Flores.clip_image003West Ham walikuwa na nafasi hadi hii leo Saa 10 Jioni, Bongo Taimu, kuwajulisha FA nia yao kama wanataka kupinga Kadi hiyo na baada kufanya hivyo taratibu zinawapa Masaa mengine 24 ya kutayarisha na kuwasilisha Ushahidi wao kuipinga Kadi Nyekundu hiyo.

Juzi,mara baada ya Mechi, Meneja wa West Ham Sam Allardyce alimlaani Chico Flores kwa kusababisha Andy Carroll atolewe na kudai wataikatia Rufaa Kadi hiyo.

Baada West Ham kukata Rufaa, Jopo Huru la Watu Watatu litakaa na kupitia ushahidi wa pande zote, Marefa na West Ham, na pia kuangalia Mkanda wa Video wa Tukio lenyewe na kisha kutoa uamuzi.

Ikiwa Rufaa itatupwa nje, Carroll atatumikia Kifungo cha Mechi 3 na kuzikosa Mechi za Timu yake dhidi ya Aston Villa, Norwich na Southampton.

Mechi hiyo na Swansea ilikuwa Mechi ya 3 tu kwa Carroll kurudi Uwanjani baada kuwa Majeruhi kwa karibu Miezi 8 na ni yeye ndie alietengeneza Bao zote mbili zilizofungwa na Kevin Nolan walipoichapa Swansea Bao 2-0.

MATA ADAI GUNDU LITAISHA!clip_image002Mchezaji mpya wa Mabingwa Manchester United, Juan Mata, amedai bahati mbaya iliyowasakama itaisha hivi karibuni.

Juzi Man United walikikwaa kipigo cha 8 kwenye Ligi Kuu England walipofungwa 2-1 na Stoke City huku Robin van Persie, Wayne Rooney na Mata wakianza Mechi ya kwanza pamoja kwa mara ya kwanza.

Lakini Mata anaamini bahati mbaya itaisha na amesema: “Bahati mbaya hatukushinda Mechi yetu ya pili Wiki hiyo. Ni Uwanja mgumu na upepo mkali haukusaidia kucheza Soka. Lakini hatukustahili kufungwa!”

Aliongeza: “Tulikuwa na bahati mbaya kwa Goli lao la kwanza, tukarudisha na tulijua tutashinda lakini tukafungwa la pili kwa Bao la bahati pia. Tulipata nafasi nzuri hatukuzitumia. Lakini tunahisi hatuwezi kufungwa tena Gemu kama hizi. Natumai ile bahati iliyotoweka kwetu itarudi tena kwani tuna bahati mbaya hata kwenye Majeruhi. Tulipoteza Masentahafu wawili kabla Haftaimu. Lakini naamini tutaanza mbio za ushindi na kuwa bora zaidi!”

LIGI KUU ENGLAND RATIBA MECHI ZIJAZO:

 

Jumamosi Februari 8

1545 Liverpool v Arsenal

1800 Aston Villa v West Ham

1800 Chelsea v Newcastle

1800C rystal Palace v West Brom

1800 Norwich v Man City

1800 Southampton v Stoke

1800 Sunderland v Hull

2030 Swansea v Cardiff

 

Jumapili Februari 9

1630 Tottenham v Everton

1900 Man United v Fulham

 

Jumanne Februari 11

2245 Cardiff v Aston Villa

2245 Hull v Southampton

2245 West Ham v Norwich

2300 West Brom v Chelsea

 

Jumatano Februari 12

2245 Arsenal v Man Unitwd

2245 Everton v Crystal Palace

2245 Man City v Sunderland

2245 Newcastle v Tottenham

2245 Stoke v Swansea

2300 Fulham v Liverpool

MSIMAMO:

NA

TIMU

P

GD

PTS

1

Arsenal

24

26

55

2

Man City

23

42

53

3

Chelsea

23

23

50

4

Liverpool

24

29

47

5

Everton

24

12

45

6

Tottenham

24

-1

44

7

Man Utd

24

10

40

8

Newcastle

24

1

37

9

Southampton

24

7

35

10

Aston Villa

24

-7

27

11

Stoke

24

-14

25

12

Swansea

24

-6

24

13

Hull

24

-7

24

14

Sunderland

24

-11

24

15

Norwich

24

-18

24

16

Crystal Palace

24

-18

23

17

West Brom

24

-6

23

18

West Ham

24

-9

22

19

Cardiff

24

-22

21

20

Fulham

24

-31

19

CREDIT TO SOKA IN BONGO

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top