FACEBOOK YATIMIZA MIAKA 10, ILIANZISHWA FEB4, 2004

clip_image001Jumanne ya Jana, February 4, Facebook imetimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake.
Kampuni hiyo ya mtandao wa kijamii iliingiza mapato ya zaidi ya dola bilioni 2.5 katika robo tatu ya mwaka 2013.
Facebook ilianzishwa, tarehe 4, February 2004 na Mark Zuckerberg pamoja na wenzake waliokuwa wakisoma pamoja kwenye chuo kikuu cha Harvard ambao ni pamoja na Eduardo Saverin, Andrew McCollum, Dustin Moskovitz na Chris Hughes.
Hadi September mwaka jana, Facebook ilikuwa na watumiaji zaidi ya bilioni 1.2 duniani kote.
Je wewe Ulisherekeaje ukiwa ni miongoni mwa watu zaidi ya Bilioni 1.2 katika hii dunia, Hebu tueleze au ulipitwa bila kujua?


Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post